NEWS
BLOG
NEWS
Monday, November 26, 2012
TIMU YA RWNANDA ILIYOKO KATIKA MASHINDANO LEO IMEWEZA KUIBUKA NA USHINDI WA MABAO2-0,MAGOLI ALIYEFUNGA NI MSHAMBULIAJI WA, WA TIMU YA YOUNG AFRICAN SPORT CLUB NIYONZIMA DAKIKA 79.

TIMU YA RWNANDA ILIYOKO KATIKA MASHINDANO LEO IMEWEZA KUIBUKA NA USHINDI WA MABAO2-0,MAGOLI ALIYEFUNGA NI MSHAMBULIAJI WA, WA TIMU YA YOUNG AFRICAN SPORT CLUB NIYONZIMA DAKIKA79

Sunday, November 25, 2012
![]() |
JOHN BOCCO,NDIYE ALIYEFUNGA MAGOLI YOTE2-0. |
MSUVA AKIMTOKA MCHEZAJI WA SUDAN. |
MASHABIKI WA TANZANIA WAKIJA KUWAPA SUPPORT TIMU YAO. |
TIMU ya soka ya taifa ya Tanzania Bara, imeanza vema kampeni zake za kuwania Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge, baada ya kuichapa mabao 2-0 Sudan katika mchezo uliomalizika usiku huu kwenye Uwanja wa Mandela, Namboole, Kampala, Uganda.
Ushindi huo, unaiweza Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars katika nafasi ya pili kwenye msimamo wa Kundi B, nyuma ya Burundi inayoongoza kwa wastani wa mabao.
Hadi mapumziko, Stars walikuwa mbele kwa mabao 2-0, yote yakipachikwa kimiani na mshambuliaji wa Azam FC, John Raphael Bocco ‘Adebayor’ aliyetumia vema krosi za Mrisho Khalfan Ngassa.
Bocco alifunga bao la kwanza Bocco aliiwahi vema krosi ya Ngassa aliyewatoka mabeki wa Sudan wingi ya kushoto na kuitumbukiza kimiani dakika ya 14.
Adebayor wa Chamazi aliwainua tena vitini mashabiki wa Tanzania dakika ya 28, akiunganisha krosi ya Ngassa tena kutoka kule kule kushoto.
Kwa ujumla Tanzania Bara walicheza vizuri kipindi cha kwanza, wakishambulia zaidi kupitia pembeni, kulia Simon Msuva ambaye hakuwa na madhara sana na kushoto Ngassa ambaye alikuwa mwiba mchungu haswa kwa Wasudan.
Pamoja na Bara kutawala kipindi cha kwanza, lakini Wasudan walifanya mashambulizi kadhaa ya kushitukiza na sifa zimuendee mlinda mlango Juma Kaseja, ambaye alioko amichomo miwili ya hatari mno.
Kipindi cha pili Stars, inayofundishwa na Mdenmark Kim Poulsen iliendelea kutawala mchezo, lakini safu ya ulinzi ya Sudan iligangamala.
Tanzania Bara; Juma Kaseja, Erasto Nyoni, Amir Maftah, Shomari Kapombe, Kevin Yondan, Frank Domayo, Salum Abubakar/Amri Kiemba, John Bocco, Mwinyi Kazimoto na Simon Msuva/Shaaban Nditi.
Sudan; Ebd Elrahman Ali, Moawia El Amin, Sami Abdallah, Faris Abdallah, Hamoda Bashir/Farid Mohamed, Mohamed El Mortada, Sadam Abutalib, Mohamed Mussa Idris, Modathir Mohamed, Adam Sayer/Osama El Rashid na Mohamed Osman/Saed Siddig.
Katika mchezo wa awali, Burundi walishinda mabao 5-1, mabao yake yakifungwa na Chris Nduwarugira dakika ya 35 na 88, Yussuf Ndikumana dakika ya 41 na Suleiman Ndikumana dakika ya 84 na 90, wakati la Somalia lilifungwa na Mohamed Jabril kwa penalti dakika ya 55.
Matokeo hayo yanalifanya Kundi B lizidi kuwa gumu, kwani Burundi inaongoza kwa pointi zake tatu na mabao mengi, Tanzania ya pili kwa pointi tatu na mabao mawili- lakini bado Sudan wanaweza kupata matokeo mazuri katika mechi zijazo.
NENO LA LEO LANGU
MUNGU BARIKI TANZANIA MUNGU BARIKI WACHEZAJI WAKE.
Saturday, November 24, 2012
TIMU ya
taifa ya Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars imelalamikia Uwanja mbovu wa Chuo
Kikuu cha Kampala Kampasi ya Biashara, waliopelekwa kufanya mazoezi leo
kujiandaa na mechi ya kesho ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati,
CECAFA Tusker Challenge 2012 dhidi ya Sudan, itakayopigwa kwenye Uwanja wa
Mandela, Namboole mjini hapa.
Ofisa Habari
wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniphace Wambura amewasilisha malalamiko
hayo kwa Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Uganda (FUFA), Rodgers Mulindwa
ambaye ameahidi kuyafanyia kazi.
“Tutalifanyia
kazi suala hilo, tutakuwa na kikao kesho litawasilishwa na litapatiwa usumbufu,
mwanzo huwa na matatizo, lakini mambo yatakuwa mazuri,”alisema
Mulindwa.
Hata hivyo,
inashangaza Stars kupelekwa katika Uwanja wa Chuo Kikuu cha Kampala Kampasi ya
Biashara, wakati kwenye mpango wa awali kabisa wa FUFA ilitakiwa kufanya mazoezi
kwenye Uwanja wa Nakawa.
Kwa upande
wake, kocha wa Kilimanjaro Stars, Mdenmark Kim Poulsen amesikitishwa na
kutowasili kwa washambuliaji Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu wa TP Mazembe ya
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).
“Mbwana
Samatta na Thomas Ulimwengu wanaweza wasicheze katika mechi ya kesho kwa sababu
hawajafika, lakini mimi nikiwa kocha nimejiandaa vizuri na nina imani na
wachezaji waliopo,” alisema.
“Nina imani
TFF wanafuatilia suala hili na wachezaji hawa watajiunga na wenzao hivi karibuni
lakini hii haituzuii kufanya vizuri kwani tumejiandaa vizuri,”
alisema.
Alisema
wachezaji wote wana hali nzuri na wana ari ya kushinda mechi yao ya kwanza dhidi
ya Sudan ambazi zimo katika Kundi B pamoja na Burundi na Somalia
Friday, November 23, 2012
UMOJA wa
wanamichezo waliowahi kucheza klabu mbalimbali zikiwemo za Ligi Kuu ya Soka
Tanzania Bara wenye maskani yao mjini Bukoba, Kagera, Bukoba Veteran Sports Club
ni katika kuhamasisha ushiriki wa timu za Tanzania, Kilimanjaro Stars na
Zanzibar Heroes, kwenye michuano ya Kombe la Tusker Challenge inayofanyika
jijini Kampala Uganda, umeandaa safari ya mashabiki walioko mkoani humo Kanda ya
Ziwa kwa ujumla kwenda kushangilia mechi za timu
hizo.Katibu Mkuu
wa Bukoba Veterans, Shijja Richard ameiambia BIN ZUBEIRY leo kwamba kwa kuanzia,
mashabiki hao wataondoka mjini Bukoba Jumapili Novemba 25, 2012 kwenda
kuishangilia timu ya taifa ya Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars katika mechi yake
ya kwanza ya michuano hiyo dhidi ya Sudan
Kaskazini.Amesema nia
na madhumuni ya safari hiyo ni kuhamasisha wachezaji wa timu za taifa za
Tanzania waweze kufanya vizuri katika michuano hiyo mikubwa kwenye ukanda wa
Afrika Mashariki na Kati na kutoa hamasa kwa watanzania kujenga tabia ya
kushangilia timu zao na pia wanadhani kuwa ushiriki wao utaongeza ushindani
katika michuano hiyo.Amesema
tayari taratibu zote zimeshafanyika ikiwa ni pamoja na kuwasiliana na Shirikisho
la Soka la Tanzania (TFF) ili wawasiliane na mamlaka zinazohusika kwa ajili ya
kupatiwa eneo maalumu uwanjani litakalowezesha watanzania waweze kuishangilia
vizuri timu ya taifa.
“Tunatarajia
kwenda uwanjani na zaidi ya mashabiki 60 ambao hivi sasa wanakamilisha taratibu
za mwisho za kuvuka mpaka wa nchi. Matarajio yetu ni kuendelea kuziunga mkono
timu za taifa katika michuano hiyo hadi kufikia mwisho wa michuano. Tunaomba
watanzania wengine walioko kanda ya ziwa katika mikoa ya Shinyanga, Mara na
Mwanza watuunge mkono,”alisema Richard.Kikosi cha
kinatarajiwa kuwasili leo mjini Kampala, kikitokea Mwanza tayari kwa mashindano
hayo ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Tusker Challenge
2012 yanayotarajiwa kuanza kesho.Stars
imekuwa kambini mjini Mwanza kwa takriban wiki mbili sasa ikijifua vikali chini
ya kocha wake, Mdenmark Kim Poulsen kujiandaa kwenda kutwaa taji la nne la
Challenge.Kikosi cha Kilimanjaro Stars kilichopo kambini mjini
Mwanza, kinaundwa na makipa; Juma Kaseja
(Simba SC) na Deogratius Mushi ‘Dida’ wa Azam FC, mabeki; Kevin Yondan (Yanga),
Erasto Nyoni (Azam FC), Issa Rashid (Mtibwa Sugar), Shomari Kapombe na Amir
Maftah (Simba).
Viungo ni
Salum Abubakar ‘Sure Boy’ (Azam FC), Amri Kiemba, Mwinyi Kazimoto, Ramadhan
Singano ‘Messi’ na Mrisho Ngassa (Simba), Athuman Iddi ‘Chuji’, Frank Domayo
(Yanga) na Shaaban Nditi (Mtibwa Sugar) wakati washambuliaji ni John Bocco
‘Adebayor’ (Azam FC), Simon Msuva (Yanga), Christopher Edward (Simba), Mbwana
Samatta na Thomas Ulimwengu wa (TPM, DRC).Bara ambayo inajivunia kutwaa mara tatu Kombe la
Challenge katika miaka ya 1974, 1994 na 2010 na kushika nafasi ya pili mara
tano, imepangwa Kundi B pamoja na Sudan,
Burundi na Somalia.
Itaanza
kampeni zake Novemba 25 kwa kumenyana na Sudan saa 12:00 jioni, mchezo
utakaotanguliwa na mechi kati ya Burundi na Somalia itakayoanza saa 9:00 Alasiri
kabla ya kurudi tena dimbani, Novemba 28 kukipiga na Burundi, mchezo
utakaotanguliwa na mechi kati ya Somalia na
Sudan.Stars
iatahitimisha mechi zake za kundi hilo kwa kumenyana na Somalia Desemba 1,
mchezo utakaotanguliwa na mechi nyingine kati ya Sudan na Burundi. Mechi zote za
Stars zitakuwa saa 12:00 jioni.
MAKUNDI
RATIBA TUSKER CHALLENGE 2012:KUNDI A: Uganda, Kenya, Ethiopia na Sudan
Kusini
KUNDI B:
Tanzania, Sudan, Burundi na Somalia
KUNDI C:
Malawi, Eritrea, Rwanda na Zanzibar
RATIB KUNDI
A:Novemba 24,
2012:
Ethiopia v
Sudan (Saa 9:00 Alasiri)Uganda v
Kenya (Saa 12:00
jioni)Novemba 27,
2012:
Sudan Kusini
v Kenya (Saa 9:00 Alasiri)Uganda v
Ethiopia (Saa 12:00
jioni)Novemba 30,
2012:
Kenya v
Ethiopia (Saa 9:00 Alasiri)Sudan Kusini
v Uganda (Saa 12:00 jioni)
RATIBA KUNDI
B:Novemba 25,
2012:
Burundi v
Somalia (Saa 9:00 Alasiri)Tanzania v
Sudan (Saa 12:00
jioni)Novemba 28,
2012:
Somalia v
Sudan (Saa 9:00 Alasiri)Tanzania v
Burundi (Saa 12:00
jioni)Desemba 1,
2012:
Sudan v
Burundi (Saa 9:00 Alasiri)Somalia v
Tanzania (Saa 12:00
jioni)
RATIBA KUNDI
C:Novemba 26,
2012:
Zanzibar v
Eritrea (Saa 9:00 Alasiri)Rwanda v
Malawi (Saa 12:00 jioni)Novemba 29,
2012:
Malawi v
Eritrea (Saa 9:00 Alasiri)Rwanda v
Zanzibar (Saa 12:00
jioni)Desemba 1,
2012:
Malawi v
Zanzibar (Saa 9:00 Alasiri)Eritrea v
Rwanda (Saa 12:00
jioni)
ROBO
FAINALI:Desemba 3, 2012Mshindi
Kundi C vs Mshindi wa Pili Kundi B (Saa 10:00
jioni)Mshindi
Kundi A vs Mshindi wa Tatu Bora wa pili (Saa 1:00
usiku)Desemba 4, 2012 (16:00):
Mshindi
Kundi B vs Mshindi wa Tatu Bora wa kwanza (Saa 10:00
jioni)Mshindi wa
Pili Kundi A vs Mshindi wa Pili Kundi C (Saa 1:00
usiku)
NUSU
FAINALI:
Desemba 6,
2012Nusu Fainali
ya Kwanza (Saa 10:00 jioni)Nusu Fainali
ya Pili (Saa 1:00
usiku)
MSHINDI WA
TATU:
Desemba 8, 2012Waliofungwa
Nusu Fanali (Saa 10:00 jioni)
FAINALI:
Desemba 8, 2012Walioshinda
Nusu Fainali (Saa 1:00 usiku)
x
MZUNGUKO wa
pili wa Ligi Kuu ya Soka ya Tanzania Bara huko mashakani kufanyika baada ya
Mapato ya Taifa(TRA) kuzifunga akaunti za udhamini wa ligi
hiyo.
TRA
ilizifunga akaunti za TFF ikiwemo ya udhamini wa ligi hiyo ikiwa ni sehemu ya
kulishinikiza Shirikisho la Soka nchini(TFF) kulipa makato ya kodi kwenye
mishahara ya timu ya taifa(Taifa Stars) tokea kipindi cha kocha Marcio
Maximo.
Akizungumza
na waandishi wa habari jana Kaimu Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka nchini(TFF)
Sunday Kayuni alisema mishahara ya makocha wa Taifa Stars tangia kocha Marcio
Maximo ilikuwa haikatwi kodi na hivyo kufanya gharama wanazodaiwa na mamlaka ya
Mapato kufikia shilingi milioni 157,407.968.00.
Alisema
wamekuwa wakipata taarifa ya mara kwa mara toka TRA ikiwakumbusha juu ya makato
hao na wao kuwajibu kuwa hawahusiki kwenye malipo ya mishahara ya makocha hao
kwani ni waajiriwa wa Serikali.
Kayuni
alisema hata hivyo kwa kuwa wao ndio walezi wa makocha hao TRA imeamua kuzifunga
akaunti zao ikiwemo ya udhamini wa Ligi Kuu ya Soka ya Tanzania Bara ambayo ina
zaidi ya shilingi milioni 300.
Alisema
kutokana na hali hiyo walifanya mazungumzo ya mara kwa mara na TRA bila ya
mafanikio na kuamua kuunda kamati itayoshirikisha Kamati ya Ligi ikishirikiana
na Wizara ya Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo kwa ajili ya kufanya
mazungumzo na mamlaka hiyo ya mapato nchini.
“Tunaona
labda tukiunganisha nguvu zetu labda wenzetu wa TRA wanaweza kutusikiliza, hivyo
Kamati tutakayounda kwa kushirikiana na wizara itakwenda kujaribu kufanya tena
mazungumzo na TRA.”alisema Kayuni.
Kwenye
Mkutano huo na waandishi wa habari Kayuni aliambatana na Makamu Mwenyekiti wa
Kamati ya Ligi Kuu Saidi Mohamedi na Mkurugenzi Mkuu wa Ligi Kuu ya Soka ya
Tanzania Bara Silas Mwakibinga, ambao wote walionyesha umuhimu wa kuunganisha
nguvu zao kuishawishi TRA.
MAMBO yameiva Yanga- matumaini ya wapenzi wa klabu hiyo kushuhudia klabu yao ikiwa na Uwanja mpya wa kisasa yameanza kuonyesha dalili za kutimia, kufuatia uongozi wa klabu hiyo kusaini makubaliano ya awali na Kampuni ya Beijing Construction Engineering Group iliyojenga Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kwa ajili ya ujenzi wa Uwanja wa Kaunda.Mwenyekiti wa mabingwa hao wa Afrika Mashariki na Kati, Alhaj Yussuf Mehboob Manji leo amesaini makubaliano na Meneja Mkuu wa Kampuni hiyo, David Zhang, makao makuu ya klabu hiyo, makutano ya mitaa ya Jangwani na Twiga, Dar es Salaam.Katika makubaliano hayo, ujenzi huo wa Uwanja utakaokuwa na uwezo wa kuchukua mashabiki 30,000 hadi 40,000 utaanza rasmi Juni mwakani.Akizungumza na Waandishi wa Habari wakati wa kusaini makubaliano hayo leo mchana, Alhaj Manji alisema kwamba wanfurahi kuanza safari ya ujenzi wa Uwanja wao na anaamini huo ni mwanzo wa mzuri wa mipango yao ya kuifanya Yanga ijitegemee kiuchumi.Katika hatua nyingine, Manji amesema kwamba katika mipango yao ya kuifanya Yanga ijimudu kiuchumi, wanafikiria kulikarabati pia jengo dogo la klabu hiyo, liliopo Mtaa wa Mafia.Alhaj Manji alisema Jumatatu kampuni hiyo ya ujenzi kutoka China, ambayo ndiyo iliyojenga Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam itachukua vipimo kwenye Uwanja wa Kaunda na Uongozi wa Yanga kuliwasilisha suala la ujenzi huo kwenye Mkutano Mkuu wa Wanachama wa klabu hiyo, Desemba 8, mwaka huu.Alisema baadhi ya fedha kwa ajili ya uwanja huo wa kisasa watakapo benki na gharama nyingine zitatokana na michango ya wanachama baada ya kuwa wamepata gharama nzima za ujenzi za uwanja huo.Meneja Mkuu wa Kampuni ya Beijing Cobnstruction Engineering Group alisema wanafurahia kufikia makubaliano ya awali ya ujenzi wa uwanja na klabu ya Yanga.Alisema wao ndio walijenga Uwanja wa Taifa na viwango vya ujenzi vya uwanja huo vilisifiwa na timu ya taifa ya Brazil iliyokuja kucheza mechi ya kirafiki na Tanzania mwaka 2010 ikiwa njiani kuelekea Afrika Kusini ambako fainali za kombe la Dunia zilifanyika.
Subscribe to:
Posts (Atom)